Wednesday, September 3, 2014
KOMPANY HATARINI KUKOSA PAMBANO LA LEO KATI YA UBELGIJI NA AUSTRALIA.
Vicent Kompan.
Nahodha wa timu ya taifa ya Ubelgiji na klabu ya Manchester City Vicent Kompan anataraji kufanyiwa vipimo vya nyama za paja baada ya kuumia akiwa mazoezini leo na kikosi chake cha timu ya taifa.
Kocha mkuu wa Ubelgiji Marc Wilmots mlinzi huyo mwenye umri wa miaka 28 amewahishwa hospitali kwa uchunguzi zaidi na yupo kwenye hatihati ya kukosa pambano la leo la kirafiki dhidi ya Australia.
Kocha huyo amesema nahodha huyo aliyesajiliwa na Man City mwaka 2008 akitokea Hambarg anauwezekano mkubwa wa kulikosa pambano hilo kama atakuwa ameumia sana ili kumuepusha na maumivu makali zaidi.
Kompan ambaye amekuwa mhimili mkubwa katika nafasi ya ulinzi ya mabingwa wa ligi kuu ya England Manchester City kiasi cha kuisaidia kutwaa ubingwa wa ligi mara mbili msimu wa 2011/2012 pamoja na msimu wa 2013/2014.
Mkule.blogsport.com
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment