Torres akiwa na kocha Jose Mourinho.
Kocha mkuu
wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho amesema alimtaka mshambuliaji wa timu hiyo Fernando
Torres kujiunga na Inter Milan badala ya AC Milan zote za nchini Italia katika
msimu wa usajili uliomalizika hivi karibuni.
Mourinho
ambaye ni raia wa Ureno amesema alitaka Torres ahamie Inter lakini hata
kujiunga kwake na AC Milan ni uamuzi mzuri na ataweza kuisaidia vyema timu hiyo
ambayo imekimbiwa na mshambuliaji Mario Balotelli aliyejiunga na Liverpool ya
England.
Kocha huyo
amesistiza kuwa mshambuliaji huyo anauwezo mzuri hivyo kujiunga kwake na AC Milan kutampa
fursa yakuonesha kipaji alichonacho ambacho kiliyumba tangu ajiunge na Chelsea
kwa ada ya paund milioni 50 mwezi januari mwaka 2011 akitokea Liverpool.
Torres
ambaye ni raia wa Hispania amejiunga na AC Milan kwa mkopo wa
miaka miwili akitokea kwa matajiri wa jiji la Londond Chelsea siku
chache kabla ya dirisha la usajili kufungwa.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment