Caroline wozniacki
Mchezaji
Caroline Wozniacki amefuzu kuingia hatua ya robo fainali ya mashindano ya wazi
ya Marekani kufuatia kupata ushindi dhidi ya mchezaji nambari tano kwenye
mchezo wa tenesi duniani kwa upande wa wanawake Maria Sharapova.
Wozniacki
anayeshikiria nafasi ya kumi kwenye mchezo huo duniani amepata ushindi dhidi ya
Sharapova baada ya kufunga seti 6kwa4 , seti2kwa6, seti 6kwa2 licha ya mchezo kuwa
wa upinzani mkali.Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24, amefuzu hatua hiyo ikiwa ni muda mrefu tangu mwaka 2012 ashiriki mashindano hayo na kuondoshwa katika hatua ya awali na kwa hivi sasa anajiandaa kukabili ana na Sara Errani kutoka Italia.
Sharapova ambaye amewahi kuwa bingwa wa zamani wa mashindano ya wazi ya Marekani kwa mwaka 2011 ameungana na Simona Halep pamoja na Ana Ivanovic walioondoshwa mapema katika hatua ya awali ya mashindano hayo.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment