Pages

Ads 468x60px

Tuesday, September 23, 2014

SANTOS KOCHA MPYA WA TIMU YA TAIFA YA URENO.



                                  Fernando Santos kocha mpya wa timu ya taifa ya Ureno.

Shirikisho la soka nchini Ureno FRF limemtangaza Fernando Santos kuwa kocha mpya wa timu yao ya taifa  kuchkua mikoba ya Paulo Bento aliyejiuzulu hivi karibuni  baada ya kufungwa na Albania kwenye mchezo wa kufuzu mataifa ya Ulaya EURO 2016.
Santos ambaye ni kocha wa zamani wa vilabu vya Fc Port na Benfica  ameifundisha timu ya taifa ya Ugiriki kwa miaka 4  na kuiwezesha kufika nusu fainali ya Euro 2012 huku akiivusha nchi hiyo hatua ya 16 bora kwenye kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil kabla ya kutolewa kwa matuta na Costa Rica.
Ureno  inataraji kucheza mchezo wa kirafiki na Ufaransa October 11 mjini Paris kabla ya kusafiri kuivaa Denmark  katika raundi ya pili ya kufuzu fainali za mataifa ya Ulaya siku tate baadae.
Santos aliachia kibarua cha kuifundisha Ugriki siku mmoja baada ya kuondoshwa kwenye fainali za kombe la dunia mwaka huu  kabla ya mazungumzo ya kupewa mkataba  mkataba mpya kufanyika.
                             Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment