Kocha mkuu wa mabingwa wa La liga Atletico madrid Diego Semeone.
Kocha mkuu wa mabigwa wa ligi kuu ya Hispania Atletico Madrid Diego Semeone amemsifu mshambuliaj Arda Turan kwa uwezo mzuri aliouonyesha katika pambano la usiku wa jana dhidi ya Real Madrid ambapo timu yake ilishinda magoli 2 kwa1.
Mchezaji huyo ambaye aliingia dakika ya 61 kuchukua nafasi Gabi aliifungia Atletico Madrid goli la pili na la ushindi dakika ya 76 baada ya kazi nzuri iliyofanywa na Juanfran nakuifanya timu hiyo kuibuka na ushindi wa magoli hayo 2 kwa1.
Semeone ambaye ni raia wa Argentina amesema katika mchezo huo timu yake ilicheza vyema kipindi cha kwanza lakini hakufurahishwa na walivyoanza kipindi cha pili lakini alifurahishwa sana na kazi aliyoifanya Turan akitokea bench na kuwapaushindi.
Katika mchezo huo Atletico Madrid ilijipatia magoli yake kupitia kwa Tiago na Arda
Turan huku
Real Madrid waliokuwa nyumbani Santiago Bernabeu kupata goli la kufutia machozi
kupitia kwa mchezaji Cristiano Ronaldo.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment