Sunday, September 7, 2014
PLATIN:KAMA BLATTER ATAENDELEA NA URAIS WA FIFA 2019 SOKA LITAZIDI KUWA HATARINI.
Rais wa Uefa Michel Platin
Rais wa shirikisho la soka barani Ulaya Uefa Michel Platin amesema mchezo huo duniani utakuwa na maaendeleo mabaya kama rais wa sasa wa Fifa Sepp Blatter atagombea tena nafasi hiyo katika uchaguzi ujao utakachofanyika mwaka 2019.
Platin ambaye ni raia wa Ufaransa amesema kwajinsi anavyomfahamu Blatter hatoshangaa kuona kiongozi huyo mkubwa wa soka duniani aking’ang’nia madaraka na jambo hilo ndilo linalolitafuna soka kwasasa.
Kuhusiana na kashfa ya rushwa iliyowakumba wajumbe wa FIFA juu ya Qatar kuandaa fainali za kombe la dunia mwaka 2022 Platin amesema licha tuhuma hizo ushahidi ndio njia pekee ya kutambua ukweli na hilo.
Akizungumzia teknolojia mbalimbali kutumika katika soka hususani ile ya magoli rais huyo wa Uefa amesema yeye sio muumini wa vifaa kama hicho kwakuwa kinapunguza ladha ya soka na haya yote yanachangiwa kwakiasi kikubwa na Blatter.
Mkule.blogsports.com
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment