Monday, September 15, 2014
ANCELOTTI: SINASHAKA NA KIBARUA CHANGU.
Carlo Ancelotti.
Kocha mkuu wa klabu ya Real Madrid ya Hispania Carlo Ancelotti amesema hana hofu yeyote juu ya kibarua chake licha ya timu hiyo kupata matokeo mabaya hivi karibuni katika ligi kuu ya La Liga.
Ancelotti ambaye ni raia wa Italia amesema pamoja na sasa kuwa kwenye wakati mgumu anaamini timu yake itaimarika kwakuwa inawachezaji wazuri ambao wanauwezo wa kuleta matokeo mazuri siku za usoni.
Kocha huyo ambaye ataiongoza Real Madrid kesho kwenye mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi klabu bingwa Ulaya dhidi ya Fc Basel amesema matumaini ya kutetea ubingwa wao wa Ulaya yapo pamoja na ushindani mkubwa unaoonekana kuwepo msimu huu.
Kocha huyo wa zamani wa Chelsea amesema zipo timu zimeimarika hususani Chelsea ya Uingereza baada ya kusajili wachezaji kama Diego Costa, Cesc Fabregas, Filipe Luis na ujio wa mlindamlango Thibaut Courtois umezidisha kasi ya klabu hiyo ya London.
Mkule.blogsport.com
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment