Cristiano Ronaldo.
Mshambuliaji wa Real Madrid ya Hispania Cristiano Ronaldo amesema bado anatamani siku mmoja arudi kuichezea timu yake ya zamani ya Manchester
United katika siku zijazo za soka lake.
Ronaldo ambaye ni raia wa Ureno amebainisha kuwa anaipenda Manchester
United na kila mtu anafahamu hilo kwakuwa mara nyingi amekuwa akizungumza suala la kuipenda timu hiyo na mapenzi hayo yanatoka moyoni mwake.
Pamoja na kukiri kuwa na furaha akiwa Real Madrid baada ya kudumu kwa zaidi ya miaka mine sasa tangu ajiunge nayo mwaka 2009 akitokea Man United amesema daima anaikumbuka timu yake ya zamani kutokana na kuwa na marafiki wengi zaidi.
Licha ya Manchester United kuanza vibaya msimu huu wa ligi kuu ya Uingereza mshindi huyo wa tuzo ya mchezaji bora dunia na ulaya kwasasa amesema usajili wa Radmel Falcao na Angel di Maria utairudisha United kwenye hadhi yake iliyozoeleka.
Mkule.blogsport.com
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment