Wednesday, September 17, 2014
MUSTAKABALI WA UCHAGUZI WA NFF NI SEPTEMBER 20 MWAKA HUU.
Shirikisho la soka la nchini Nigeria NFF linataraji kufanya mkutano tarehe 20 ya mwezi huu mjini Warri kwaajili ya kupanga utaratibu wa uchaguzi kupata viongozi wapya baada ya Fifa kutoa agizo hilo.
Kwamujibu wa katibu mkuu wa shirikisho la mpira wa miguu nchini Nigeria Musa Amadu amesema kikao hicho kitahudhuriwa na wawakilishi wa vyama mbalimbali kama chama cha waamuzi,chama cha makocha na chama cha wachezaji.
Amadu amesema kikao hicho ndicho kitakachochagua wajumbe wa kamati mbalimbali za uchaguzi huo pamoja na kupanga siku ya uchaguzi na eneo utakapo fanyika kabla ya mwezi huu kumalizika.
Amadu amebainisha kuwa mkutano huo utakaojumuisha wajumbe 36 wa NFF utahudhuriwa na mwaklishi kutoka fifa na kila kitu kitakuwa wazi ili kuondoa wasiwasi uliyopo miongoni mwa watu juu ya utendaji wa shirikisho hilo.
Mkule.blogsport.com
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment