Mr.Liverpool Steven Gerald.
Hatua ya
makundi ya michunao ya klabu bingwa barani Ulaya inaanza leo kwa vilabu 16
kushuka viwanjani huku Liverpool ikiionja michuano hiyo kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2009 ambapo timu hiyo ilishiriki
kwa mara ya mwisho.
Ikiwa
imepita miaka mitano tangu washiriki kwa mara ya mwisho Liverpool chini ya
kocha Brendan Rogers watakuwa nyumbani Anfield kuikaribisha timu ya Ludogorits kutoka nchini Bulgaria.
Miongoni mwa michezo ya leo timu ya Arsenal
itakuwa ugenini kuikabili Borussia Dortmund wakati Olympiakos ya Ugiriki
itakuwa ikiikaribisha Atletico Madrid ya Hispania huku mabingwa watetezi Real
Madrid watakuwa nyumbani kuialika Fc Basel ya Uswis.
Michezo yote kuanza saa tatu na dkk 45 usiku.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment