Daniel Sturridge akigangwagangwa na daktari wa timu yake ya taifa ya England.
Klabu ya Liverpool ya Uingereza inataraji kumkosa mshambuliaji wake Daniel Sturridge kwa muda wa majuma sita baada ya kuuumia mwenyewe akiwa mazoezini kwenye timu yake ya taifa.
Kocha mkuu wa Liverpool Brendan Rodgers amethibitisha kuwa mshambuliaji huyo alieumia mazoezini akiwa kwenye timu yake ya taifa ya Uingereza alibainika kuumia saa 36 baada ya kucheza dakika 89 kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya Norway juma lililopita.
Sturridge anataraji kukosa michezo 6 ya ligi ukiwemo dhidi ya watani wao wa jadi Everton utakaochezwa tarehe 27 ya mwezi huu,pambano dhidi ya Middlesbrough wa kombe la ligi pamoja na mchezo wa kwanza hatua ya makundi klabu bingwa Ulaya.
Kuumia kwa Sturridge aliyejiunga na Liverpool akitokea
Chelsea kunatoa nafasi kwa mshambuliaji
mpya wa timu hiyo Mario Ballotelli kuwa
kwenye uwezekano mkubwa wa kucheza mchezo wake wa kwanza kesho wakati Liverpool itakapoikaribisha Aston Villa.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment