Frank Ribery.
Mshambuliaji wa Bayern munich Frank
Ribery amesema kamwe hawezi kubadili uamuzi wake wa kustaafu soka la kimataifa
baada ya kutangaza uamuzi huo siku kadhaa zilizopita.
Ribery mwenye umri wa miaka 31
uamuzi wake wa kustaafu kuitumikia timu ya taifa ya Ufaransa umekosolewa na
rais wa shirikisho la soka barani Ulaya Michel Platini ambaye hivi karibuni
amesema anaweza kumwadhibu winga huyo ikiwa atagoma kuchezea timu ya taifa kama
ataitwa na kocha Didier Dischamps.
Pamoja na kushambuliwa vikali na
rais huyo ambaye ni raia wa Ufaransa Ribery ambaye alikosa fainali za kombe la
dunia mwaka huu kutokana na kusumbuliwa na jeraha la nyama za paja amesema
kwasasa akili yake ameielekeza kwenye klabu yake ambayo inakibarua cha kutetea
taji la Bundesiliga msimu huu.
"I want to focus completely on
Bayern Munich in the future. That's all I want to say about the matter. I am
not going to get involved in all the politics surrounding my decision."
Mchezaji huyo amesema ameshazungumza
na kocha wa timu ya Ufaransa Didier Deschamps juu ya uamuzi wake wa kustaafu na
wamekubaliana hivyo hana mpango wa
kurudi kuichezea timu ya taifa.
Katika michezo 81 aliyoichezea timu
ya taifa ya Ufaransa mchezaji huyo amefunga magoli 16
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment