Nicolas Anelka.
Mshambuliaji wa zamani wa vilabu vya Real Madrid,PSG,Chelsea na Arsenal Nicolas Anelka anajiandaa kujiunga na klabu ya FC Pune City baada ya kuamua kughairi kujiunga na Mumbai City.
Licha ya mchezaji huyo wa zamani wa timu ya taifa ya Ufaransa kuvivutia vilabu mbalimbali vya nchini India lakini yeye ameamua kujiunga na timu ya Mumbai City ya Maharashtra nchi iliyopo magharibi mwa India.
Anelka mwenye umri wa miaka 35 tangu afukuzwe na timu yake ya zamani yaWest Bromwich Albion ya England amekosa klabu ya kuchezea licha ya mara kadhaa kuhusishwa na mipango ya kujiunga na timu mbalimbali ikiwemo za nchini Brazil.
Mkongwe huyo ambaye pia amewahi kuvichezea vilabu vya Juventus na Manchester City mwaklishi wake amekuwa kwenye mazungumzo na timu ya FC Pune City kwaajili ya kukubaliana juu ya usajili huo.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment