Monday, September 8, 2014
ENGLAND YAENDELEA KUANDAMWA NA MAJERUHI,HENDERSON HATARINI KUIVAA USWIS LEO.
Jordan Henderson
Kiungo wa timu ya taifa ya Uingereza Jordan Henderson yupo kwenye hatihati ya kuukosa mchezo wa kufuzu kwa fainali za kombe la mataifa ya Ulaya mwaka 2016 dhidi ya Uswis unataraji kuchezwa leo .
Habari kutoka katika kambi ya timu ya taifa ya Uingereza zimeeleza kuwa kiungo huyo yupo kwenye hatari kutocheza pambano hilo litakalochezwa kwenye uwanja wa St.Jacob Park mjini Basel baada ya kuumia kifundo cha mguu akiwa mazoezini.
Nyota wa Manchester City Jemes Milner huenda akachukua nafasi ya Henderson licha ya mchezaji Fabian Delph anayeichezea Aston Villa kuonyesha uwezo mkubwa kwenye pambano la hivi karibuni ambapo Uingereza ilicheza na Norway.
Mbali na Jordan Henderson kuwa kwenye hatarai ya kuukosa mchezo huo wa leo kocha wa Ungereza Roy Hodgson amewaengua mlindamlango Ben Foster na kiungo Jack Colback kutokana na kuwa majerihi.
Mkule.blogsport.com
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment