Andy Murry.
Bingwa wa zamani wa
mashindano ya wazi ya Marekani anayeshikiria nafasi ya 9 duniani kwa upande wa
wanaume Andy Murray amefuzu kuingia hatua ya robo fainali ya mashindano hayo baada ya kumshinda
mpinzani wake Jo-Wilfried Songa.
Murray,
ambaye katika mashindano hayo anashikiria nafasi ya nane amepata ushindi
huo kufuatia kumshinda Songa kwa seti
7kwa5, seti7kwa5, seti 6kwa4 ikiwa ni miaka mitatu ipite tangu afuzu
kuingia hatua ya robo fainali mwaka 2010.
Mchezaji nambari moja
duniani Novak Djokovic amefuzu kuingia hatua ya robo fainali kufuatia kupata
ushindi kutoka kwa mpinzani wake Philipp Kohlschreiber ambaye ni mwenyeji wa
mashindano hayo.
Kwa upande wa wanawake mwanadada Serena
Williams anajiandaa kukabiliana na
Flavia Pennetta kwenye hatua ya robo fainali ya mashindano ya wazi ya
Marekani baada ya kumfunga mpinzani wake Kaia Kanepi kwa seti 6kwa3,seti 6kwa3
kwa dakika65.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment