Paulo Bento.
Shirikirisho
la soka nchini Ureno limethibitisha kuwa aliyekuwa kocha mkuu wa timu ya taifa hilo
Paulo Bento ameachia ngazi baada ya kikosi chake kufungwa na Albania kwenye
mchezo wa kufuzu fainali za mataifa ya Ulaya mwaka 2016.
Bento mwenye
umri wa miaka 45 amefikia makubaliano na shirikisho la soka la nchi hiyo ya kukatisha mkataba kufuatia kipigo cha goli
1 kwa 0 kutoka kwa Albania mapema juma hili na mchakato wa kumtafuta
mrithi wa nafasi yake umeanza.
shirikisho
hilo la soka la Ureno FPF limemshukuru
kocha huyo kwa mchango wake wa kuifundisha timu yao nakusema wanamatumaini kuwa watapata kocha
mwengine atakekuwa na jukumu la kuifundisha timu hiyo siku chache kutoka sasa.
Bento ambaye
alicheza michezo 35 kwenye timu ya taifa
ya Ureno akiwa mchezaji alianza kuinoa
Ureno mwaka 2010 akichukua nafasi ya Carlos Queiroz ambaye aliachia ngazi
kutokana na kuanza vibaya kwenye michezo
ya kufuzu kwa fainali za Ulaya 2012.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment