Monday, September 8, 2014
MAICON KUUKOSA MCHEZO WA KESHO KATI YA BRAZIL NA EQUADOR.
Mlinzi wa timu ya taifa ya Brazil Doglas Maicon jezi namba 2.
Mlinzi wa klabu ya AS Roma ya Italia Doglas Maicon ameachwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Brazil kinachojiandaa kuikabili Equador kesho jumanne na nafasi yake kuchukuliwa na nyota wa AS Monaco Fábio Tavares maarufu kama Fabinho.
Maicon ambaye alianzishwa na kocha Dunga katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Colombia ijumaa iliyopita imeelezwa anamatatizo ambayo hata hivyo hayajawekwa wazi na kocha wa kikosi hicho kijulikanao kama Selecao.
Taarifa za kuenguliwa kwa mlinzi huyo wa zamani wa vilabu vya Inter Milan na Manchester City zimethibitisha mapema usiku wa kuamkia leo na kocha wa sasa wa Brazil aliyechukua nafasi ya Luis Felipe Scolar.
Mrithi wa Maicon Fabinho amewasili asubuhi ya leo katika kambi ya timu ya taifa ya Brazil tayari kwa mchezo huo wa kesho dhidi ya Equador.
Mrithi wa Maicon katika timu ya Fabinho.
Mkule.blogsport.com
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment