Nicolas Anelka
Nyota wa zamani wa vilabu vya soka
vya Chelsea , Real Madrid, na Arsenal
Nicolas Anelka ametangaza kujiunga na klabu ya
Mumbai City inayoshiriki ligi kuu ya nchini India baada ya kukaa bila
timu tangu aachwe na West Bromwich ya Uingereza.
Anelka mwenye umri wa maiak 35
ametangaza kupitia ukurasa wake wa kijamii wa Twita akisema anamatumaini kuwa atapewa ushirikiano mkubwa na wachezaji
kwenye timu yake mpya na atahakikisha
anacheza kwa kujituma katika michezo atakayocheza.
Mkongwe huyo ambaye amecheza michezo
69 katika timu yake ya taifa ya Ufaransa alianzia soka lake katika klabu ya PSG kabla ya kujiunga na Arsenal na
baadae kuvichezea vilabu vya Real Madrid,Manchester City, Fenerbahce, Bolton,
Chelsea, Shanghai Shenhua, Juventus na hatimae
West Bromwich.
Anelka anaungana na wachezaji wengine
wakongwe wanaolipwa pesa nyingi kwa siku
kwenye ligi kuu ya India akiungana na Robert
Pires ,Freddie Ljungberg , Alessandro del Piero na David Trezeguet.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment