Alessio Cerci.
Mabingwa wa ligi kuu
Hispania maarufu kama La Liga Atletico
Madrid wamekubali kumsajili mshambuliaji
wa kimataifa wa Italia Alessio Cerci kutoka klabu ya Torino inayoshiriki ligi
kuu ya kwao.
Cerci mwenye umri wa miaka 27 anataraji kusaini mkataba wa miaka
mitatu na mabingwa hao baada ya kufuzu
vipimo vya afya kabla ya dirisha la usajili kufungwa rasmi leo huku akitegemewa
kuchukua nafasi ya Diego costa. Mchezaji huyo ambaye msimu huu alishiriki michuano ya kombe la dunia nchini Brazil amekuwa akiwaniwa na vilabu mbalimbali barani Ulaya ikiwemo klabu ya Arsenal pamoja na Manchester United.
Mkurugenzi wa michezo wa Atletico Madrid Jose caminero ameeleza kuwa wamefurahi kufikia makubaliano na mchezaji huyo atakayekuwa msaada mkubwa katika kikosi chao kwenye msimu huu wa ligi kuu Hispania.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment