Radmel Falcao.
Wakati dirisha la usajili
barani Ulaya likitaraji kufungwa rasmi usiku wa leo klabu ya Manchester United imefikia
makubaliano na Monaco ya Ufaransa juu ya kumsajili kwa mkopo wa muda mrefu mshambuliaji
Radmel Falcao.
Falcao ambaye ni raia wa Colombia uhamisaho
wake wa kutua Manchester United umegharimu kiasi cha paundi milioni 6 na ataraji kufanyiwa vipimo kabla ya dirisha
la usajili kufungwa majira ya saa sita na dakika moja usiku wa leo.
Tangu ajiunge na Monaco ya
Ufaransa kwa paundi milioni 50 mwezi mei
2013 Falcao kwa msimu uliopita amefunga magoli 11 katika michezo 20 aliyocheza
na mitatu ya msimu huu .
Falcao ambaye amekuwa akihusishwa na mipango
ya kujinga na Arsenal vyombo vya habari baranu Ulaya vimearifu kuwa kocha wa
Manchester United Louis Van Gaal ameanza kumfuatilia mshambuliaji huyo tangu
saa 48 zilizopita.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment