Pages

Ads 468x60px

Sunday, September 14, 2014

MAYWEATHER AMCHAKAZA MAIDANA LICHA YA KUNG'ATWA KIDOLE.




Mwanamasumbwi raia wa Marekani Floyd Mayweather ameendelea kushikilia ubingwa wa WBA na WBC baada ya kumshinda kwa pointi  bondia Marcos Maidana mjini Las Vegas Marekani.
Mayweather mwenye umri wa miaka 37 ameendeleza rekodi katika miaka 18 ya  maisha yake ya ngumi akicheza michezo 47 bila kupoteza ukilinganisha na mabondia wengine tangu aanze kushiriki ngumi za kuliwa mwaka 1996.
Bondia huyo ameweka rekodi ya kushinda michezo 47 kwenye ngumi za kulipwa,akishinda mipambano 26 kwa K.O  huku mipambano mitano mikubwa ya dunia akishikilia ubingwa na kutopigwa pambano lolote.

Akizungumza mara baada ya mchezo Mayweather  mwenye uzito wa kilo 68 amesema hakuamini pale ambapo mpinzani wake alimng’ata kidole chake katika mzunguko wa nane jambo lilomfanya asitumie sana mkono wake wa kushoto.
Floyd Mayweather factfile
Born: 24 February 1977, Grand Rapids, Michigan
Amateur record: 84 wins, six defeats. Three-weight Golden Gloves champion. Bronze medal at 1996 Olympics
Turned professional: 11 October 1996
Professional record: 47 wins (26 KOs), no defeats. Five-weight world champion
Worth: Highest-paid athlete in world in 2012, earning $85m (all from boxing), and 2014, earning $105m (all from boxing)


Ushindi huo umeripotiwa kumpatia Mayweather  takribani dola za marekani milioni 32 sawa na paundi milioni 19.6 kwa pambano hilo liliokuwa likisubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa masumbwi duniani kote.


                                           Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment