Kocha mkuu
wa timu ya taifa ya Ujerumani Joachim Low amemteua mchezaji Bastian Schweinsteiger kuwa nahodha mpya baada ya kustaafu kwa
nahodha wa awali Philipp Lahm mwezi
uliopita.
Wakati Schweinsteiger
akipewa unahodha kocha Joachim Low amesema uamuzi wa kumteua kiungo huyo kuwa
nahodha mpya unatokana na sifa ya uongozi akiwa ndani na hata nje ya uwanja
hivyo anaimani naye huku msaidizi wake akiwa Manuel Neur.
Kocha huyo
amesema benchi la ufundi zima limekuwa na imani na mchezaji huyo mwenye umri wa
maiak 30 na akiwa amecheza michezo 100 kwenye timu ya taifa tangu mwaka 2004.
Schweinsteiger
atakosa mchezo wa kirafiki dhidi ya
Argentina unaotaraji kuchezwa hivi
karibuni kutokana na kuwa majeruhi hivyo
mlinda mlango Manuel Neur ambaye ni nahodha msaiodizi atakuwa na jukumu hilo la kuwaongoza wenzake .
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment