Pages

Ads 468x60px

Wednesday, September 17, 2014

QUEIROZ AONGEZA MKATANA WA KUIONOA TIMU YA TAIFA YA IRAN.



                                         Carlos Queiroz.

Kocha wa zamani wa Ureno na klabu ya Real Madrid ya Hispania Carlos Queiroz amefikia makubaliano ya kuiongeza mkataba   mpya wa miaka minne kuendelea kuifundisha timu ya taifa ya Iran.
Kocha huyo ambaye aliiongoza Iran mwaka huu kwenye fainali za kombe la dunia  nchini Brazil  alikuwa kwenye hatihati ya kuongeza mkataba mpya kwakile kilichoelezwa hakuwa na maelewano na baadhi ya viongozi wa shirikisho la soka la Iran.
Queiroz ambaye ni mzaliwa wa Msumbiji amesema  hapendi kuahidi atafanyaje katika timu hiyo ya taifa lakini mikakati yake ni kuiongoza vyema  kwenye michuano ya mataifa ya barani Asia  itakayofanyika mwezi ujao nchini Australia.
Iran ambayo imelitwaa taji hilo kwa mara ya mwisho mwaka 1976 imepangwa kundi C lenye mataifa ya United Arab Emirates, Bahrain  na  Qatar huku kocha Queiroz akiahidi pia kuisaidia nchini Iran kufuzu fainali za kombe la dunia mwaka 2018

                              Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment