Carlos Queiroz.
Kocha wa zamani wa Ureno na klabu ya Real Madrid ya Hispania Carlos Queiroz amefikia makubaliano ya kuiongeza mkataba mpya wa miaka minne kuendelea kuifundisha timu ya taifa ya Iran.
Kocha huyo ambaye aliiongoza Iran mwaka huu kwenye fainali za kombe la dunia nchini Brazil alikuwa kwenye hatihati ya kuongeza mkataba mpya kwakile kilichoelezwa hakuwa na maelewano na baadhi ya viongozi wa shirikisho la soka la Iran.
Queiroz ambaye ni mzaliwa wa Msumbiji amesema hapendi kuahidi atafanyaje katika timu hiyo ya taifa lakini mikakati yake ni kuiongoza vyema kwenye michuano ya mataifa ya barani Asia itakayofanyika mwezi ujao nchini Australia.
Iran ambayo imelitwaa
taji hilo kwa mara ya mwisho mwaka 1976 imepangwa kundi C lenye mataifa ya
United Arab Emirates, Bahrain na Qatar huku kocha Queiroz akiahidi pia
kuisaidia nchini Iran kufuzu fainali za kombe la dunia mwaka 2018
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment