Wednesday, September 17, 2014
KIBARUA CHA OLE GUNNAR HATARINI KUOTA NYASI.
Ole Gunnar Solskjaer.
Kocha wa timu ya Cardiff City Ole Gunnar Solskjaer amekutana na uongozi wa klabu hiyo kwalengo la kufanya mazungumzo juu ya matokeo mabaya waliyoyapata katika michezo ya Championship.
Kikao hicho kinafuatia vipigo viwili mfululizo ambavyo timu hiyo imevipata ndani ya siku nne ikifungwa 1 kwa 0 na Middlesbrough jana jumanne pamoja na ule wa capitulation dhidi ya Norwich ambapo timu hiyo ilifungwa magoli 4 kwa 2.
Solskjaer mwenye umri wa miaka 41 alichukua mikoba ya Malky Mackay January 2 kwaka huu lakini alishindwa kuinusuru timu hiyo na janga la kushuka daraja katika ligi kuu ya Uingereza.
Mshambuliaji huyo mkongwe wa Manchester United amesema anakubali lawama zote zinazoelekezwa kwake kutokana na matokeo mabaya waliyoyapata lakini akisistiza kuwa kikosi hicho kitapata matokeo mazuri hivi karibuni.
Katika michezo 30 aliyoiongoza Cardiff City kuanzia achukue nafasi hiyo kocha huyo ameshinda michezo 9 akienda sare 5 na kupoteza michezo 16 hali ambayo inatishia kibarua chake kuota nyasi.
Mkule.blogsport.com
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment