Magoli ya washindi kwenye mchezo huo wa kundi A yametiwa kimiani na mchezaji Joackins Atudo kwa penalti dakika ya sita na mshambuliaji wa AFC Leopards ya Kenya, Allan Wanga kunako dakika ya 60.
Katika mchezo mwingine uliochezwa leo timu ya soka ya Sudani kusini imeyaaga mashindano hayo baada ya kufungwa magoli 2 kwa 0 na Ethiopia pambano lililochezwa kwenye uwanja wa Afrah uliopo mjini Nakuru.
Magoli ya Ethiopia yamefungwaYousuf Yassin na Biruk Kalbolre.
Sudan kusini imeyaaga mashindano hayo bila kushinda mchezo wowote katika kundi lake la A.
Michuano hiyo inataraji kuendelea tena kesho ambapo timu ya taifa ya Tanzania bara Kilimanjaro stars itakuwa uwanjani kucheza na Burundi huku Somalia ikiikabili Zambia Chipolopo michezo ambayo itatoa taaswira ya nani ataongoza kundi hilo huku vita kali ikiwa ni kwa Zambia,Burundi na Kili Stars.
Huu ni msimamo wa kundi B.
Group B
# | Team | MP | W | D | L | F | A | D | P | Last 5 matches | H2H | |
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
1 | Tanzania | 2 | 1 | 1 | 0 | 2 | 1 | +1 | 4 | W D | ||
2 | Zambia | 2 | 1 | 1 | 0 | 2 | 1 | +1 | 4 | W D | ||
3 | Burundi | 2 | 1 | 0 | 1 | 2 | 1 | +1 | 3 | L W | ||
4 | Somalia | 2 | 0 | 0 | 2 | 0 | 3 | -3 | 0 |
mkule.blogspot.com
No comments:
Post a Comment