Timu
ya tifa ya Tanzania bara Kilimanjaro stars imetinga rasmi robo fainali ya michuano ya Challenge baada ya leo kuinyuka Burundi goli 1 kwa 0
katika mchezo uliochezwa nchini Kenya.
Bao
pekee la Kili stars limefungwa na Mbwana Samata dkk 7 nakuifanya timu hiyo
kutoka Tanzania bara kuingia moja kwa mmoja hatua mhimu ya michuano hiyo
iliyoanza November 27 ikishirikisha mataifa wanachama wa Cecafa.
Kwa matokeo
hayo, Kilimanjaro stars imemaliza ikiwa
na alama 7 baada ya awali kushinda goli 1-0 dhidi ya Somalia na kutoka sare
ya kufungana goli 1 kwa1 na mabingwa wa zamani wa Afrika timu ya taifa ya Zambia Chipolopolo.
ya kufungana goli 1 kwa1 na mabingwa wa zamani wa Afrika timu ya taifa ya Zambia Chipolopolo.
Mchezo
unaoendelea hivi sasa ni kati ya Somalia ambao wapo nyuma kwa magoli 3 kwa 0
dhidi ya timu ya taifa ya Zambia
Chipolopolo.
Kwajinsi hali ilivyo
uwezekano ni mkubwa mno kwa Zambia kuuungana na Kilimanjaro stars kuingia hatua
ya robo fainali ya mashindano hayo kutoka kunda B.
mkule.blogspot.com
No comments:
Post a Comment