Pages

Ads 468x60px

Sunday, December 8, 2013

ZAMBIA NA SUDANI ZATINGA NUSU FAINALI MICHUANO YA CHALLENGE.



Timu za taifa za Zambia Chipolopolo na Sudani zimefanikiwa kufuzu hatua ya nusu fainali kwenye michuano ya kombe la Challenge inayoendelea huko nchini Kenya kwakushirikisha mataifa wanachama wa Cecafa.
Katika michezo ya robo fainali iliyochezwa leo kwenye mashindano hayo timu ya taifa ya Sudani imefanikiwa kutinga nusu fainali baada ya kuifunga Ethiopia magoli 2 kwa 0.
Katika mchezo wa awali hii leo Zambia iliitoa Burundi kwa changamoto ya Penalti baada ya kuifunga penalty 4 kwa 3 hii ikiwa ni baada ya kutoka suluhu ya kutofungana katika muda wa dakika 90.
Kwamatokeo hayo Zambia na Sudani zinaungana na Kilimanjaro Stars pamoja na wenyeji Kenya kutinga hatua hiyo mhimu ambayo itategua kitendawili cha nani na nani wataingia fainali.

No comments:

Post a Comment