Timu za taifa za Zambia Chipolopolo
na Sudani zimefanikiwa kufuzu hatua ya nusu fainali kwenye michuano ya kombe la
Challenge inayoendelea huko nchini Kenya kwakushirikisha mataifa wanachama wa
Cecafa.
Katika michezo ya robo fainali iliyochezwa
leo kwenye mashindano hayo timu ya taifa ya Sudani imefanikiwa kutinga nusu
fainali baada ya kuifunga Ethiopia magoli 2 kwa 0.
Katika mchezo wa awali hii leo
Zambia iliitoa Burundi kwa changamoto ya Penalti baada ya kuifunga penalty 4
kwa 3 hii ikiwa ni baada ya kutoka suluhu ya kutofungana katika muda wa dakika
90.
Kwamatokeo hayo Zambia na Sudani
zinaungana na Kilimanjaro Stars pamoja na wenyeji Kenya kutinga hatua hiyo mhimu
ambayo itategua kitendawili cha nani na nani wataingia fainali.
No comments:
Post a Comment