Arena Corinthians
Jumla ya viwanja vitatu kati ya
vinavyojengwa nchini Brazil kwaajili ya fainali za kombe la dunia havitakuwa
tayari kukamilika katika muda uliopangwa na shirikisho la soka duniani Fifa.
Viwanja hivyo vya Arena Pantanal
uliopo kwenye mji wa Cuiaba,Arena da Baixada uliopo Curitiba na Arena
Corinthians uliopo Sao Paulo havitakuwa vimekamilika hadi kufikia December 31
Fifa imethibitisha hilo.
Ujenzi wa viwanja vyote
vitakavyotumika kwenye fainali za mwakani nchini Brazil unatakiwa kukamilika
hadi kufikia tarehe 31 ya mwezi huu pamoja na kukumbwa na maafa ya kuporomoka
kwa dhaadhi ya viwanja kiasi cha kupoteza maisha ya watu.
Uwanja uliopo Sao Paulo mwezi
uliopita ulisababisha vifo vya watu wawili wanaume waliokuwakwenye ujenzi wa
dimba la Arena Corinthians ambalo upo kweenye orodha ya viwanja vitatu
vitakavyoshindwa kukamilika katika muda uliopangwa na fifa.
Arena Pantanal uliopo kwenye mji wa Cuiaba.
mkule.blospot.com
No comments:
Post a Comment