Bosi wa klabu ya Manchester City Manuel
Pellegrin amekanusha vikali habari kuwa mshambuliaji Edin Dzeco anaweza kuuzwa
mwezi januari mwakani katika msimu wa usajili barani Ulaya.
Katika taarifa yake Pellegrin amesema nyota
huyio mwenye umri wa miaka 27 atabakia kuwa mmoja wa watakaoendelea
kuitumikia klabu hiyo yenye maskani yake
jijini Manchester nay eye binafsi hayupo tayari kumpoteza msjhambuliaji huyo.
Pellegrin amesema ni jambo la mhimu sana kwa
timu yake kuwa na kikosi imara kwakuwa wanakabiliwa na michezo mingi ya kucheza
kwasasa hadi mwezi wan ne mwakani na kama wanahitaji mataji sharti wawe na
wachezaji wazuri.
Haya ni maneno ya Pellegrin akisistiza
kutompiga bei Dzeco "Maybe at the
moment he is not playing as much as he would like, but he remains an important
part of the squad."
Kauli ya kocha huyo alieiwezesha City kufuzu
hatua ya 16 bora kwenye michuano ya klabu bingwa barani Ulaya msimu huu itakuwa
ni mwiba mkali kwa mashabiki wa vilabu vya Arsenal,
Borussia Dortmund na Inter Milan ambavyovimekuwa katika vita ya kutaka saini
yake.
Dzeco amefunga magoli 7 katika michezo 14
aliyocheza msimu huu kwenye mashindano yote lakini amekuwa na mwanzo mbaya
msimu huu wa ligi kuu ya England tangu mwishoni mwa mwezi September mwaka huu.
mkule.blogspot.com
No comments:
Post a Comment