Kiungo wa klabu ya soka ya Manchester City na
timu ya taifa ya Ivory coast Yaya Toure ametangazwa mshindi wea tuzo ya
mchezaji bora wa Afrika kwa mwaka wa 2013 katika tuzo zinazotolewa na shirika
la utangazaji la BBC.
Yaya ambaye ameingia katika kinyang’anyiro
hicho kwa miaka minne amewashinda wachezaji Pierre-Emerick Aubameyang, Victor
Moses, John Mikel Obi na Jonathan
Pitroipa ambao wote kwa pamoja
wameshindwa kutamba mbele yake.
Akizungumza mara baada
ya kupata tuzo hiyo Yaya mwenye umri wa miaka 30 hivi sasa amesema amefarijika
sana kuwa mshindi wa tuzo hiyo baada ya kuingizwa kwenye kinyang’anyiri hicho
mara nne bila mafanikio lakini mara ya tano amekuwa mshindi.
Ameongeza kuwa ni mafanikio makubwa kwake
kuwa mchezaji bora wa Afrika akiwaburuza nyota wa kiafrika kama Aubameyang,
Pitroipa, Mikel, Moses, Salomon Kalou, Gervinho ambao kwasasa wanatamba katika
soka la kimataifa.
- 2012 - Christopher Katongo (Zambia and Henan Construction)
- 2011 - Andre 'Dede' Ayew (Marseille & Ghana)
- 2010 - Asamoah Gyan (Sunderland & Ghana)
- 2009 - Didier Drogba (Chelsea & Ivory Coast)
- 2008 - Mohamed Aboutrika (Al Ahly & Egypt)
- 2007 - Emmanuel Adebayor (Arsenal & Togo)
- 2006 - Michael Essien (Chelsea & Ghana)
- 2005 - Mohamed Barakat (Al Ahly & Egypt)
- 2004 - Jay Jay Okocha (Bolton & Nigeria)
- 2003 - Jay Jay Okocha (Bolton & Nigeria)
- 2002 - El Hadji Diouf (Liverpool & Senegal)
- 2001 - Sammy Kuffour (Bayern Munich & Ghana)
- 2000 - Patrick Mboma (Parma & Cameroon)
Mbali na kutoa mchango mkubwa kwa klabu yake
ya Manchester City kwenye ligi kuuu ya England na katika michuano ya klabu
bingwa Ulaya Yaya amekuwa msaada mkubwa kuiwezesha Ivory Coast kuwa miongoni
mwa mataifa matano ya Afrika yatakayoshiriki fainali zijazo za kombe la dunia
zitakazofanyika mwakani nchini Brazil.
mkule.blogspot.com
No comments:
Post a Comment