Timu ya taifa ya Rwanda
Amavubi leo imejiweka pabaya katika michuano ya kombe la Challenge baada ya
kufungwa goli 1 kwa 0 na Sudani mchezo uliochezwa kwenye dimba la nyasi bandia
la City mjini Nairobi Kenya.
Alikuwa ni mchezaji Salah
Ibrahim aliyewakatisha tama Wanyarwanda hao baada ya kunga goli hilo pekee dkk
29 kwa shuti kali lililoenda moja kwa moja kimiani kwenye mchezo huo wa kundi
C.
Hiki ni kipigo cha pili
mfululizo inachokipata Rwanda kwenye michuano hiyo iliyoanza kutimua vumbi Nov
27 mwaka huu matokeo ambayo yanaifanya Rwanda ikose matumaini ya kutinga Robo
fainali hasa ikikumbwa kuwa walifungwa goli 1 kwa 0 na Uganda katika pambano la
awali.
Katika Pambano la pili
kwenye kundi hilo la C mabingwa watetezi Uganda wakiongozwa na nyota wao Hamisi Kiiza
na Emanueli Okwi wametinga robo fainali baada ya kuifunga Eritrea magoli 3 kwa
0.
Magoli ya Uganda hii leo
yametiwa kimiani na Emanueli Okwi aliyefunga katika dk 9 na 39 huku nyota wa
klabu ya Yanga Hamisi Kiiza akifunga goli la 3 kwamkwaju wa penalty.
Ushindi huo, unaifanya
Uganda ifikishe alama sita baada ya
awali kuifunga Rwanda goli 1-0 na kupanda kileleni mwa Kundi hilo kwa wastani
wa mabao, kwani hata Sudan ina pointi sita.
Michuano hiyo inataraji
kuengelea tena kesho Sudani kusini ikiikabili Ethiopia huku wenyeji Kenya
wakichuana na Zanzibar Heros.
MSIMAMO WA MAKUNDI YOTE BAADA YA MICHEZO YA LEO NI KAMA IFUATAVYO:-
Group C
# | Team | MP | W | D | L | F | A | D | P | Last 5 matches | H2H | ||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
1 | Sudan | 2 | 2 | 0 | 0 | 4 | 0 | +4 | 6 | W W | |||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
2 | Uganda | 2 | 2 | 0 | 0 | 4 | 0 | +4 | 6 | W W | |||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
3 | Rwanda | 2 | 0 | 0 | 2 | 0 | 2 | -2 | 0 | L L | |||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
4 | Eritrea | 2 | 0 | 0 | 2 | 0 | 6 | -6 | 0 |
No comments:
Post a Comment