Klabu ya soka ya Real Betis inashiriki ligi
kuu ya Hispania imemfuta kazi kocha wake Pepe Mel baada ya kuwa na mwanzo mbaya
katika msimu huu wa La liga kiasi cha kuwafanya wakae kwenye eneo la kushuka
daraja.
Mel ambaye ameiongoza timu hiyo katika
michezo 15 msimu huu nafasi yake kuchukuliwa na kocha wa zamani wa nyambizi ya
Villareal Juan Carlos Garrido aliyetimuliwa kazi mwaka 2011.
Mel mwenye umri wa miaka 50 alianza
kuifundisha timu hiyo mwaka 2010 hadi hivi sasa alipofutwa kazi ambapo anaiacha
timu hiyo ikiwa na alama 10 katika nafasi ya 20 kwenye msimamo wa ligi kuu ya
Hispania.
mkule.blogspot.com
No comments:
Post a Comment