Uongozi wa timu
ya soka ya Bayer Leverkusen ya Ujeruman umetangaza kumfuta kazi aliyekuwa kocha
wao Sami Hyypia kufuatia timu hiyo kubugizwa magoli 2 kwa1 na Lowly Hamburg.
Uamuzi wa
kumtupia virago kocha huyo unatokana na mwenendo mbaya wa timu ambapo katika
michezo 14 imeshinda michezo 3 pekee pamoja na kipigo cha jana ijumaa dhidi ya Lowly
Hamburg.
Matokeo ya
jana yamezidi kuiweka pabaya timu hiyo katika kukata tiketi ya kushiriki ligi
ya mabingwa Ulaya msimu ujao na badala
yake nafasi ya kushiriki Uefa msimu ujao
huenda ikaangukia kwa Wolfsburg na Borussia
Monchengladbach endapo timu hizo zitashinda michezo waliyonayo mwishoni mwa
juma hili.
Hyypia ambae
alianza kuinoa Leverkusen mwezi mei 2012 taarifa zimeeleza kuwa nafasi yake
huenda ikachukuliwa na kocha wa timu ya vijana Sascha Lewandowski ambae atakuwa
akimalizia michezo ya msimu huu wa Bundesiliga.
Kiungo huyo
wa zamani wa Liverpool mwenye umri wa miaka 40 mkataba wake wasasa ndani ya
timu ya Leverkusen ulikuwa unamalizika katika msimu wa ligi mwaka 2015.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment