Pages

Ads 468x60px

Saturday, April 5, 2014

PIGO MAN UNITED,ROONEY HATARINI KUIKOSA MECHI DHIDI YA FC BAYERN MUNICH...



 

Timu ya Manchester United ya nchini England ipo kwenye hatihati ya kumkosa mshambuliaji wake Wayne Rooney katika mchezo wa marudiano dhidi ya Bayern Munich kuwania ubingwa wa Ulaya kwa upande wa vilabu.


Taarifa iliyotolewa na kocha mkuu wa timu hiyo David Moyes imesema kuwa nyota huyo mwenye umri wa miaka 28 amepata jeraha na kidole gumba cha mguu jeraha linalotishia kuukosa mchezo huo wa robo fainali.

Kwamujibu wa kocha huyo Rooney ataukosa mchezo wa leo dhidi ya Newcastle United kuwania ubingwa wa ligi kuu ya England ambapo Manchester United imekuwa na msimu mbaya kiasi cha kusota kwenye nafasi ya saba hadi sasa.


Rooney ambaye amefunga magoli thelathini kwenye michezo themanini na moja anataraji kupatiwa matibabu mwishoni mwa juma hili ili kuona kama ataweza kucheza dhidi ya Bayern Munich.

posted by Yusuph Mkule.

No comments:

Post a Comment