skip to main |
skip to sidebar
PIGO MAN UNITED,ROONEY HATARINI KUIKOSA MECHI DHIDI YA FC BAYERN MUNICH...
Timu ya Manchester United ya nchini England
ipo kwenye hatihati ya kumkosa mshambuliaji wake Wayne Rooney katika mchezo wa
marudiano dhidi ya Bayern Munich kuwania ubingwa wa Ulaya kwa upande wa vilabu.
Taarifa iliyotolewa na kocha mkuu wa timu
hiyo David Moyes imesema kuwa nyota huyo mwenye umri wa miaka 28 amepata jeraha
na kidole gumba cha mguu jeraha linalotishia kuukosa mchezo huo wa robo
fainali.
Kwamujibu wa kocha huyo Rooney ataukosa
mchezo wa leo dhidi ya Newcastle United kuwania ubingwa wa ligi kuu ya England
ambapo Manchester United imekuwa na msimu mbaya kiasi cha kusota kwenye nafasi
ya saba hadi sasa.
Rooney ambaye amefunga magoli thelathini
kwenye michezo themanini na moja anataraji kupatiwa matibabu mwishoni mwa juma
hili ili kuona kama ataweza kucheza dhidi ya Bayern Munich.
posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment